Habari za Punde

*YANGA WAWEKA MASHADA YA MAUA KWENYE MAKABURI YA MAUAJI YA KIMBARI YA 1994-RWANDA

 Mwenyekiti wa timu ya Yanga, Yusuph Manji (kulia) Mama Karume (katikati) na baadhi ya viongozi wa timu hiyo, wakiwa wamepozi wakati wakisubiri utaratibu wa kuingia katika jumba la Makumbusho ya mauaji ya Kimbari ya mwaka 1994, yaliyotokean nchini Rwanda. Timu hiyo iko nchini Rwanda kwa mwaliko wa Rais wa Rwanda, Paul Kagame, ambapo pia itacheza michezo mitatu ya kujipima nguvu na timu za nchini humo ikiwa ni sehemu ya mazoezi ya kujiweka sawa na kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu inayotarajia kuanza Septemba 15, mwaka huu.
 Viongozi na wachezaji wa Yanga, wakielekea kuingia katika jumba la Makumbusho ili kujionea makaburi hayo.
 Hapa wakipata maelezo kutoka kwa mmoja wa maofisa wa Jumba hilo la Makumbusho, kabla ya kuingia ndani.
Viongozi na wachezaji hao wakiwa na mashada ya maua, wakiinga katika jumba hilo la Makumbusho kwa ajili ya kuweka mashada ya maua. Picha zote na Saleh Ally

No comments:

Post a Comment

SUFIANIMAFOTO Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.